SERIKALI KUPITIA WIZARA YA MAJI IMEAZIMIA KUTATUA CHANGAMOTO ZA UPATIKANAJI WA HUDUMA YA MAJISAFI KWENYE KATA ZA URU MASHARIKI PAMOJA NA KIMOCHI
Serikali kupitia Wizara ya Maji imeazimia kutatua changamoto za upatikanaji wa huduma ya majisafi kwenye Kata za Uru Mashariki pamoja na Kimochi kwa kutekeleza miradi ya maji yenye thamani ya Tshs: 754,996,141.04
Katika Kata ya Uru Mashariki, Mamlaka itafanya ukarabati wa vyanzo vya Kirikuna pamoja na Ochai vinavyokwenda kuzalisha jumla ya mita za ujazo 800 kwa siku.
Sambamba na ukarabati, Mamlaka pia italaza bomba zenye vipenyo mbalimbali urefu wa kilomita 9.9.
Aidha, kwenye Kata ya Kimochi Mamlaka itatekeleza mradi wa kulaza bomba urefu wa kilomita 28.7 kwenye vijiji vya Shia, Kisaseni pamoja na Mdawi.
Mamlaka imewasilisha taarifa hiyo kwenye kikao cha pamoja baina ya viongozi wa Chama pamoja na Serikali kwa kushirikiana na Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Moshi Vijijini.
